Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Khamenei, amesema: “Tunafanya mazungumzo na waandamanaji halali, lakini hakuna manufaa ya kufanya mazungumzo na watu wanaochochea fujo na ghasia; hawa lazima wazuiliwe na kusimamishwa.”
Amefafanua kuwa watu hao ni wachochezi na mamluki wanaohusishwa na adui, waliosimama nyuma ya wafanyabiashara (waliokuwa wakifanya Maandamano halali), na wakapaza kauli mbiu zao zinazoipinga Uislamu, Iran, na Jamhuri ya Kiislamu.
Kauli hiyo imekuja katika muktadha wa kutofautisha kati ya madai halali ya raia na vitendo vya vurugu vinavyochochewa na mawakala wa nje.
Your Comment